Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 9:3 - Swahili Revised Union Version

Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa Torati wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa Torati wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 9:3
13 Marejeleo ya Msalaba  

Na yeyote atakayelaani jina la BWANA hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzaliwa, hapo atakapolaani jina la BWANA atauawa.


Lakini mtu afanyaye neno lolote kwa kusudi, kama ni mzalia, kama ni mgeni, huyo amtukana BWANA; na mtu huyo atatupiliwa mbali na watu wake.


Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake;


kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama waandishi wao.


Mmesikia kufuru yake; mwaonaje ninyi? Wote wakamhukumu kuwa imempasa kuuawa.


Amin, nawaambia, Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote;


bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele; ila atakuwa ana dhambi ya milele,


Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,


Basi, wale Waandishi na Mafarisayo wakaanza kuulizana wakisema, Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?