Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 7:29 - Swahili Revised Union Version

kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama waandishi wao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hakuwa kama waalimu wao wa sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hakuwa kama waalimu wao wa sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hakuwa kama waalimu wao wa sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama waandishi wao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 7:29
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa neno la mfalme lina nguvu; naye ni nani awezaye kumwambia huyo, Wafanya nini?


Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.


Bali mimi, hakika nimejaa nguvu kwa Roho ya BWANA; nimejaa hukumu na uwezo; nimhubirie Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.


Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.


Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya Waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.


lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.


lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.


lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,


Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;


Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.


Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.


kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.


lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.