Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Matendo 6:10 - Swahili Revised Union Version

10 lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyemwongoza wakati aliposema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyemwongoza wakati aliposema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyemwongoza wakati aliposema.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Lakini hawakuweza kushindana na ile hekima aliyopewa na Roho wa Mungu alipokuwa akisema.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.

Tazama sura Nakili




Matendo 6:10
18 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa nimejaa maneno; Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.


Lakini hakika imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi ya Mwenyezi ndiyo impayo ufahamu.


Basi sasa, nenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha utakalolinena.


Kila silaha itengenezwayo juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.


Nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema BWANA.


Lakini hapo nitakaposema nawe, nitafumbua kinywa chako, nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. Yeye asikiaye na asikie; naye akataaye na akatae; maana wao ni nyumba yenye kuasi.


Bali mimi, hakika nimejaa nguvu kwa Roho ya BWANA; nimejaa hukumu na uwezo; nimhubirie Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.


Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotayarishwa.


kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.


Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu yeyote kama huyu anavyonena.


lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.


Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu.


Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano;


Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.


Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo