Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 10:4 - Swahili Revised Union Version

Simoni Mkananayo, na Yuda Iskarioti, naye ndiye aliyemsaliti.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote aliyemsaliti Isa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote aliyemsaliti Isa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Simoni Mkananayo, na Yuda Iskarioti, naye ndiye aliyemsaliti.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 10:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Wakati huo mmoja wa wale Kumi na Wawili, jina lake Yuda Iskarioti, aliwaendea wakuu wa makuhani,


akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha.


Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulubiwe.


Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu.


Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nilikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.


Yuda Iskarioti, yule mmoja katika wale Kumi na Wawili, akaenda zake kwa wakuu wa makuhani, apate kumsaliti kwao.


Basi alipokuwa katika kusema, mara Yuda alifika, mmoja wa wale Kumi na Wawili, na pamoja naye mkutano, wakiwa na panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee.


Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskarioti, naye ni mmoja wa wale Kumi na Wawili.


Basi alipokuwa katika kusema, tazama, mkutano wa watu, na yule aitwaye Yuda, ambaye ni mmoja wa wale Kumi na Wawili, amewatangulia. Akamkaribia Yesu ili kumbusu.


Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, moyo wa kumsaliti;


Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti.


Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Kumi na Wawili.


Wakati walipoingia, wakapanda ghorofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.


ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.