Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Matendo 7:54 - Swahili Revised Union Version

Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wazee wa Baraza la Wayahudi waliposikia haya wakaghadhibika, wakamsagia meno.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Waliposikia haya wakaghadhibika, wakamsagia meno.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Matendo 7:54
13 Marejeleo ya Msalaba  

Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea; Amesagasaga meno juu yangu; Mtesi wangu hunikazia macho makali.


Asiye haki ataona na kusikitika, Atasaga meno yake na kuondoka, Matumaini ya wasio haki hupotea.


Bila heshima walinidhihaki kupindukia, Wakanisagia meno yao.


Juu yako adui zako wote Wamepanua vinywa vyao; Huzomea, husaga meno yao, Husema, Tumemmeza; Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia; Tumeipata, tumeiona.


na kuwatupa katika tanuri ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


na kuwatupa katika tanuri ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.


Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakapanga kuwaua.