Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Marko 4:28 - Swahili Revised Union Version

Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: Kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: Kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Marko 4:28
19 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.


Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.


Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu.


Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.


Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.


Maana kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.


Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua BWANA; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.


Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.


akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.


Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.


Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;


mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu;