Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 5:8 - Swahili Revised Union Version

Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Watumwa ndio wanaotutawala, wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Watumwa ndio wanaotutawala, wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Watumwa ndio wanaotutawala, wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 5:8
12 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Na alaaniwe Kanaani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.


Lakini Sanbalati, Mhoroni, na Tobia, mtumishi wake, Mwamoni, na Geshemu, Mwarabu, walitucheka, wakatudharau, wakasema, Ni nini neno hili mnalofanya? Je! Ninyi mtaasi juu ya mfalme?


Lakini watawala wa kwanza walionitangulia, wakawalemea watu, wakawatwalia chakula na mvinyo, zaidi ya shekeli arubaini za fedha; tena hata watumishi wao nao wakawatawala watu; lakini mimi sikufanya hivyo, kwa kuwa nilimcha Mungu.


Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu; Wala hapana awezaye kuokoa kutoka kwa mkono wako?


Watoto wake wako mbali na wokovu, Nao wamesongwa langoni, Wala hapana atakayewaponya.


Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane wa kuwaokoa.


Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, Akaniburura hadi pasipokuwa na wa kuniponya.


Mtumwa apatapo kuwa mfalme; Mpumbavu ashibapo chakula;


Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hakuna awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia?


Na sasa nitaifunua aibu yake mbele ya macho ya wapenzi wake, wala hapana mtu atakayemwokoa katika mkono wangu.


Maana mimi sitawahurumia tena wenyeji wa nchi hii, asema BWANA; bali, tazama, nitawatia, kila mmoja wao, mikononi mwa mwenzake, na mikononi mwa mfalme; nao wataipiga hiyo nchi, wala mimi sitamwokoa yeyote kutoka kwa mkono wao.


Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.