Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 10:7 - Swahili Revised Union Version

7 Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu; Wala hapana awezaye kuokoa kutoka kwa mkono wako?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Wewe wajua kwamba mimi sina hatia, na hakuna wa kuniokoa mikononi mwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Wewe wajua kwamba mimi sina hatia, na hakuna wa kuniokoa mikononi mwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Wewe wajua kwamba mimi sina hatia, na hakuna wa kuniokoa mikononi mwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 ingawa unajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?

Tazama sura Nakili




Yobu 10:7
35 Marejeleo ya Msalaba  

Mimi nikiwa mwovu, ole wangu! Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu; Maana nimejaa aibu Nikiyaangalia mateso yangu.


Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi, Nami ni safi machoni pako.


Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu, Najua ya kuwa mimi ni mwenye haki.


Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.


Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.


Kwani Mungu atamtupia asimhurumie; Angependa kuukimbia mkono wake.


Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?


Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia! (Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu); Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!


(Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);


Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwenye haki machoni pake mwenyewe.


Mimi ni safi, sina makosa; Sina hatia, wala hapana uovu ndani yangu;


Je! Hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki?


Basi ikawa, baada ya BWANA kumwambia Ayubu maneno hayo, BWANA akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.


Tazama, yuanyakua, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?


Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu.


Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema, Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Umenijaribu moyo wangu, umenijia usiku, Umenichunguza usione neno; Nimenuia kinywa changu kisikose,


Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane wa kuwaokoa.


BWANA, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,


Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hakuna awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia?


Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zumari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuri liwakalo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi mikononi mwangu?


Na sasa nitaifunua aibu yake mbele ya macho ya wapenzi wake, wala hapana mtu atakayemwokoa katika mkono wangu.


Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwanasimba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukua mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kuokoa.


Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.


Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.


Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi; Naua Mimi, nahuisha Mimi, Nimejeruhi, tena naponya; Wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu,


Ninyi ni mashahidi, na Mungu pia, jinsi tulivyokaa kwenu ninyi mnaoamini, kwa utakatifu, na kwa haki, bila kulaumiwa;


Mungu, Mungu BWANA, naam, Mungu, Mungu BWANA, yeye anajua, na Israeli naye atajua; kama ni katika uasi, au kama ni katika kosa juu ya BWANA, usituokoe hivi leo;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo