Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:53 - Swahili Revised Union Version

Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Walinitupa shimoni nikiwa hai na juu yangu wakarundika mawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Walinitupa shimoni nikiwa hai na juu yangu wakarundika mawe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Walinitupa shimoni nikiwa hai na juu yangu wakarundika mawe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:53
9 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, Yeremia alipokuwa ameingia katika nyumba ya shimo, na katika vyumba vya ndani; na Yeremia alipokuwa amekaa humo siku nyingi;


Na sasa unisikilize, Ee bwana wangu mfalme; maombi yangu yakapate kibali mbele yako; usinirudishe nyumbani mwa Yonathani, mwandishi, nisije nikafa humo.


Basi wakamtwaa Yeremia, wakamtupa katika shimo la Malkiya, mwana wa mfalme, lililo katika ukumbi wa walinzi; wakamshusha kwa kamba. Na mle shimoni hamkuwa na maji, ila matope tu; naye Yeremia akazama katika matope hayo.


Ee bwana wangu, mfalme, watu hawa wametenda mabaya katika mambo yote waliyomtenda Yeremia, nabii, ambaye wamemtupa shimoni; naye hakosi atakufa pale alipo, kwa sababu ya njaa; kwa kuwa hakuna mkate kabisa katika mji.


Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia mhuri kwa mhuri wake mwenyewe, na kwa mhuri wa wakuu wake, lisibadilike neno lolote katika habari za Danieli.


Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.


Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, akiwa katika tumbo la yule samaki,


akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.


Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe mhuri, pamoja na kuwaweka wale askari walinzi.