Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:51 - Swahili Revised Union Version

Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa ajili ya kuangamizwa kwa binti wa watu wangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nalia na kujaa majonzi, kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nalia na kujaa majonzi, kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nalia na kujaa majonzi, kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa ajili ya kuangamizwa kwa binti wa watu wangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:51
14 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana nitawezaje kumwendea baba yangu, na huyu kijana hayuko pamoja nami? Nisije nikayaona mabaya yatakayompata baba yangu.


Kwa sababu hiyo BWANA wa majeshi asema hivi, Tazama, nitawaadhibu watu hawa; vijana watakufa kwa upanga; wana wao na binti zao watakufa kwa njaa;


Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.


Nikitoka kwenda shambani, tazama, wako huko waliouawa kwa upanga! Na nikiingia mjini, tazama, wamo humo wanaougua kwa sababu ya njaa! Maana nabii na kuhani, wote wawili, huenda huku na huko katika nchi, wala hawana maarifa.


Nami nitawalazimisha kula nyama ya wana wao, na nyama ya binti zao, nao watakula kila mmoja nyama ya rafiki yake, wakati wa mazingira na dhiki, ambayo adui zao, na watu wale watafutao roho zao, watawatesa.


BWANA ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.


Macho yangu yamechoka kwa machozi, Mtima wangu umetaabika; Ini langu linamiminwa juu ya nchi Kwa uharibifu wa binti ya watu wangu; Kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao, Huzimia katika mitaa ya mji.


Kijana na mzee hulala chini Katika njia kuu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wameanguka kwa upanga; Umewaua katika siku ya hasira yako; Umeua, wala hukuona huruma.


Hata BWANA atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni.


Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege;


Wanawake katika Sayuni wanashikwa kwa nguvu; Na mabikira katika miji ya Yuda.