Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 59:8 - Swahili Revised Union Version

Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika mienendo yao; wamejifanyia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Njia ya amani hamwijui kamwe; njia zenu zote ni za dhuluma. Mmejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Njia ya amani hamwijui kamwe; njia zenu zote ni za dhuluma. Mmejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Njia ya amani hamwijui kamwe; njia zenu zote ni za dhuluma. Mmejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hawajui njia ya amani, hakuna haki katika mapito yao. Wameyageuza kuwa njia za upotovu, hakuna apitaye njia hizo atakayeifahamu amani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hawajui njia ya amani, hakuna haki katika mapito yao. Wameyageuza kuwa njia za upotovu, hakuna apitaye njia hizo atakayeifahamu amani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika mienendo yao; wamejifanyia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 59:8
20 Marejeleo ya Msalaba  

Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, BWANA atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli.


Watu waziachao njia za unyofu, Ili kuziendea njia za giza;


Waliopotoka katika njia zao; Walio wakaidi katika mapito yao.


Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana; Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.


Aendaye kwa unyofu ataokolewa; Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.


Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.


Hapana amani kwa waovu, asema BWANA.


Kwa maana shamba la mizabibu la BWANA wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza; akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! Aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! Alisikia kilio.


Sisi sote twanguruma kama dubu; twaomboleza kama hua; twatazamia hukumu ya haki, lakini hapana; na wokovu, lakini u mbali nasi.


Kwa sababu hiyo hukumu ya haki iko mbali nasi, wala haki haitufikii; twatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu.


Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe;


Pigeni mbio huku na huku katika njia za Yerusalemu, mkaone sasa, na kujua, na kutafuta katika viwanja vyake, kwamba mwaweza kumpata mtu mmoja, kwamba yuko mtu mmoja awaye yote atendaye kwa haki, atafutaye uaminifu; nami nitausamehe mji huo.


Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.


Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.


Wala njia ya amani hawakuijua.