Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa
Hosea 13:11 - Swahili Revised Union Version Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Kwa hasira yangu mimi nikawapa mfalme, kisha nikamwondoa kwa ghadhabu yangu. Biblia Habari Njema - BHND Kwa hasira yangu mimi nikawapa mfalme, kisha nikamwondoa kwa ghadhabu yangu. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Kwa hasira yangu mimi nikawapa mfalme, kisha nikamwondoa kwa ghadhabu yangu. Neno: Bibilia Takatifu Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa. Neno: Maandiko Matakatifu Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa. BIBLIA KISWAHILI Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu. |
Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa
Yakini sasa watasema, Hatuna mfalme; kwa maana hatumchi BWANA; na mfalme huyu je! Aweza kututendea nini?
Kwa maana wana wa Israeli watakaa siku nyingi bila mfalme, wala mtu mkuu, wala sadaka, wala nguzo, wala naivera, wala kinyago;
Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nilikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.
lakini leo mmemkataa Mungu wenu, naye ndiye awaponyaye katika misiba yenu yote na shida zenu; nanyi mmemwambia, Sivyo, lakini weka mfalme juu yetu. Basi, sasa, njoni mbele za BWANA, kwa makabila yenu na kwa maelfu yenu.
Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu.
Basi sasa, mtazameni mfalme mliyemchagua na kumtaka; tazameni, BWANA ameweka mfalme juu yenu.
Samweli akasema, Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la BWANA, BWANA naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa Israeli.
BWANA akamwambia Samweli, utamlilia Sauli hadi lini, kwa kuwa mimi nimemkataa asiwatawale Waisraeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakutuma kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.