Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hosea 8:4 - Swahili Revised Union Version

4 Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nilikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 “Walijiwekea wafalme bila kibali changu, walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 “Walijiwekea wafalme bila kibali changu, walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 “Walijiwekea wafalme bila kibali changu, walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nilikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.

Tazama sura Nakili




Hosea 8:4
20 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa hiyo mfalme akafanya shauri, akatengeneza ng'ombe wawili wa dhahabu, akawaambia watu, Ni vigumu kwenu kupanda kwenda Yerusalemu; tazama, hii ndiyo miungu yenu, enyi Israeli, iliyowapandisha kutoka nchi ya Misri.


Kila aliyetaka akamweka wakfu, ili wawepo makuhani wa mahali pa juu. Jambo hilo likawa dhambi kwa nyumba ya Yeroboamu, hata kuiharibu, na kuifuta usoni pa nchi.


Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.


Je! Mwanadamu ajifanyie miungu, wasio miungu?


Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa; jifanyieni moyo mpya na roho mpya; mbona mnataka kufa, enyi nyumba ya Israeli?


Nebukadneza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.


Efraimu aliponena, palikuwa na tetemeko; alijitukuza katika Israeli; Lakini alipokosa katika Baali, alikufa.


Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.


Na sasa wanazidi kufanya dhambi, nao wamejifanyia sanamu kwa fedha yao, naam, sanamu kwa kadiri ya akili zao; zote pia ni kazi ya mafundi; nao huzitaja hivi, Wanaume watoao dhabihu na wazibusu ndama.


Maana hakujua ya kuwa mimi ndiye niliyempa ngano, na divai, na mafuta, na kumwongezea fedha na dhahabu, walivyovitumia kwa ajili ya Baali.


Israeli ameyatupa yaliyo mema; adui watamfuatia.


Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.


Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;


Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.


Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;


Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo