Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 5:9 - Swahili Revised Union Version

Ndipo mfalme Belshaza akahangaika sana, uso wake ukambadilika, na wakuu wake wakaona fadhaa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Ndipo, mfalme Belsasari alipozidi kustuka, nao uso wake ukawa mwingine kabisa, nao wakuu wake wakapotelewa na mizungu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 5:9
12 Marejeleo ya Msalaba  

Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.


Papo hapo tetemeko liliwashika, Uchungu kama wa mwanamke azaaye.


Ulizeni sasa, mkaone kwamba mwanamume aona uchungu wa uzazi; mbona, basi, ninaona kila mtu anaweka mikono yake viunoni, kama mwanamke aliye na uchungu, na nyuso zote zimegeuka rangi?


Tumesikia habari zake; mikono yetu inalegea; dhiki imetushika, na uchungu kama wa mwanamke wakati wa kuzaa kwake.


Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikubakiziwa nguvu.


Hata katika mwaka wa pili wa kumiliki kwake Nebukadneza, Nebukadneza aliota ndoto; na roho yake ikafadhaika, akatokwa na usingizi.


Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.


Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.


Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na muungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,