Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Danieli 5:9 - Swahili Revised Union Version

9 Ndipo mfalme Belshaza akahangaika sana, uso wake ukambadilika, na wakuu wake wakaona fadhaa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Basi, mfalme Belshaza akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakuu wake wakawa na wasiwasi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

Tazama sura Nakili

Swahili Roehl Bible 1937

9 Ndipo, mfalme Belsasari alipozidi kustuka, nao uso wake ukawa mwingine kabisa, nao wakuu wake wakapotelewa na mizungu.

Tazama sura Nakili




Danieli 5:9
12 Marejeleo ya Msalaba  

Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.


Papo hapo tetemeko liliwashika, Uchungu kama wa mwanamke azaaye.


Ulizeni sasa, mkaone kwamba mwanamume aona uchungu wa uzazi; mbona, basi, ninaona kila mtu anaweka mikono yake viunoni, kama mwanamke aliye na uchungu, na nyuso zote zimegeuka rangi?


Tumesikia habari zake; mikono yetu inalegea; dhiki imetushika, na uchungu kama wa mwanamke wakati wa kuzaa kwake.


Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikubakiziwa nguvu.


Hata katika mwaka wa pili wa kumiliki kwake Nebukadneza, Nebukadneza aliota ndoto; na roho yake ikafadhaika, akatokwa na usingizi.


Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.


Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.


Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na muungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo