Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nahumu 3:11 - Swahili Revised Union Version

11 Tena utalewa, utafichwa; tena utatafuta ngome kwa sababu ya adui.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Ninewi, nawe pia utalewa; utamkimbia adui na kujaribu kujificha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Ninewi, nawe pia utalewa; utamkimbia adui na kujaribu kujificha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Ninewi, nawe pia utalewa; utamkimbia adui na kujaribu kujificha.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Wewe pia utalewa; utaenda mafichoni na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Wewe pia utalewa; utakwenda mafichoni na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Tena utalewa, utafichwa; tena utatafuta ngome kwa sababu ya adui.

Tazama sura Nakili




Nahumu 3:11
19 Marejeleo ya Msalaba  

Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.


Ingia ndani ya jabali; ukajifiche mavumbini mbele za utisho wa BWANA, mbele za utukufu wa enzi yake.


Na watu wataingia ndani ya pango za majabali, na ndani ya mashimo ya nchi, mbele za utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.


Ngojeni mstaajabu; fanyeni anasa zenu na kuwa vipofu; wamelewa wala si kwa mvinyo; wamewayawaya wala si kwa sababu ya kileo.


Na hao wanaokuonea nitawalisha nyama yao wenyewe, nao watalewa kwa kuinywa damu yao wenyewe, kama kwa mvinyo mpya; na watu wote watajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako, na Mkombozi wako ni Mwenye enzi wa Yakobo.


Nikayakanyaga makabila ya watu kwa hasira yangu, Nikawalevya kwa ghadhabu yangu, Nami nikaimwaga damu yao chini.


Tangazeni katika Yuda, hubirini katika Yerusalemu, na kusema, Pigeni baragumu katika nchi, pigeni kelele sana, na kusema, Jikusanyeni pamoja, tukaingie katika miji yenye boma.


Nami nitawalevya wakuu wake, na watu wake wenye hekima, watawala wake, na makamanda wake, na mashujaa wake; nao watalala usingizi wa milele, wasiamke, asema Mfalme, BWANA wa majeshi, ambaye jina lake ni BWANA.


Mbona tunakaa kimya? Jikusanyeni, tukaingie ndani ya miji yenye maboma, tukanyamaze humo kwa maana BWANA, Mungu wetu, ametunyamazisha, naye ametupa maji yenye uchungu tunywe, kwa sababu tumemwasi BWANA.


Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.


Nao wajapojificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta na kuwatoa toka huko; na wajapositirika katika vilindi vya bahari nisiwaone, nitamwagiza joka huko, naye atawauma.


Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa BWANA, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako.


Kwa maana kama miiba wametatana, kama walevi wamelewa, watateketezwa kama mabua makavu.


Yeye apondaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.


Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.


Hata Waisraeli walipoona ya kuwa wako katika dhiki, (maana watu walifadhaishwa), ndipo hao watu wakajificha katika mapango, na katika vichaka, na katika miamba, na katika mashimo, na katika mabirika.


Basi, hao wote wawili wakajidhihirisha mbele ya ngome ya Wafilisti, na wale Wafilisti wakasema, Kumbe! Wale Waebrania wanatoka katika mashimo walimojificha!


Tufuate:

Matangazo


Matangazo