Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nahumu 3:10 - Swahili Revised Union Version

10 Hata hivyo alichukuliwa mbali, alikwenda utumwani; watoto wake wachanga walisetwa kwenye maachano ya njia kuu zote; watu wake wenye heshima wakapigiwa kura, na wakuu wake wote wakafungwa kwa minyororo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Hata hivyo, ulichukuliwa mateka, watu wake wakapelekwa uhamishoni. Hata watoto wake walipondwapondwa katika pembe ya kila barabara; watu wake mashuhuri walinadiwa, wakuu wake wote walifungwa minyororo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Hata hivyo, ulichukuliwa mateka, watu wake wakapelekwa uhamishoni. Hata watoto wake walipondwapondwa katika pembe ya kila barabara; watu wake mashuhuri walinadiwa, wakuu wake wote walifungwa minyororo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Hata hivyo, ulichukuliwa mateka, watu wake wakapelekwa uhamishoni. Hata watoto wake walipondwapondwa katika pembe ya kila barabara; watu wake mashuhuri walinadiwa, wakuu wake wote walifungwa minyororo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Hata hivyo alichukuliwa mateka na kwenda uhamishoni. Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande kwenye mwanzo wa kila barabara. Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima, na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Hata hivyo alichukuliwa mateka na kwenda uhamishoni. Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande kwenye mwanzo wa kila barabara. Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima, na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Hata hivyo alichukuliwa mbali, alikwenda utumwani; watoto wake wachanga walisetwa kwenye maachano ya njia kuu zote; watu wake wenye heshima wakapigiwa kura, na wakuu wake wote wakafungwa kwa minyororo.

Tazama sura Nakili




Nahumu 3:10
17 Marejeleo ya Msalaba  

Hazaeli akasema, Bwana wangu analilia nini? Akajibu, Kwa sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana wa Israeli; utazichoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawasetaseta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua.


Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima, Na kufanya biashara ya rafiki yenu.


Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.


Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.


Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma.


Na watoto wao wachanga watavunjwavunjwa mbele ya macho yao, nyumba zao zitatekwa nyara, na wake zao watanajisiwa.


Pigeni kelele za hofu; maana siku ya BWANA i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu.


Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, BWANA wa majeshi.


vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawachukua uchi, wafungwa wa Misri, na watu wa Kushi waliohamishwa, watoto kwa wazee, bila viatu, matako yao wazi, Misri iaibishwe.


Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa mikesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; Kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa, Mwanzo wa kila njia kuu.


Jinsi dhahabu ilivyoacha kung'aa, Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika! Mawe ya patakatifu yametupwa Mwanzo wa kila njia.


Walipokushika kwa mkono wako, ulivunjika, ukawararua mabega yao yote; nao walipokutegemea, ulivunjika, ukawatetemesha viuno vyao vyote.


Samaria atachukua hatia yake; kwa maana amemwasi Mungu wake; wataanguka kwa upanga; watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande, na wanawake wao wenye mimba watatumbuliwa.


Nao wamewapigia kura watu wangu; na mvulana wamemwuza ili kupata kahaba, na msichana wamemwuza ili kupata divai, wapate kunywa.


Haya ndiyo asemayo BWANA; Kwa makosa matatu ya wana wa Amoni, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili wapate kuongeza mipaka yao;


Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpigia kura Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo