Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 13:20 - Swahili Revised Union Version

20 Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Anayeandamana na wenye hekima hupata hekima, lakini anayejiunga na wapumbavu atapata madhara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Anayeandamana na wenye hekima hupata hekima, lakini anayejiunga na wapumbavu atapata madhara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Anayeandamana na wenye hekima hupata hekima, lakini anayejiunga na wapumbavu atapata madhara.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima, bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima, bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

20 Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

Tazama sura Nakili




Methali 13:20
27 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamtwaa Lutu, mwana wa nduguye Abramu, aliyekaa huko Sodoma, na mali yake, wakaenda zao.


Na wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakasema, Uwaambie hivi watu wale waliokuambia, wakisema, Baba yako alilifanya zito kongwa letu, bali wewe utufanyie jepesi, uwaambie hivi, Kidole changu cha mwisho ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.


Lakini akaliacha shauri lile la wazee, walilompa, akataka shauri kwa wale vijana waliokua pamoja naye, na kusimama mbele yake.


Ikawa wakuu wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Huyo ndiye mfalme wa Israeli Wakageuka juu yake ili wapigane naye; naye Yehoshafati akapiga kelele.


Akamwambia Yehoshafati, Je! Utakwenda nami tupigane na Ramoth-gileadi? Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako na farasi wangu ni kama farasi wako.


Lakini akaliacha shauri lile la wazee walilompa, akataka shauri kwa wale vijana wa rika yake, waliokuwa washauri wake.


Yehu mwana wa Hanani mwonaji akatoka kwenda kumlaki, akamwambia mfalme Yehoshafati, Je! Imekupasa kuwasaidia waovu, na kuwapenda wamchukiao BWANA? Kwa ajili ya hayo ghadhabu itokayo kwa BWANA i juu yako.


Akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA kama nyumba ya Ahabu; kwa kuwa hao walikuwa washauri wake, baada ya kifo cha baba yake, hata aangamie.


Mimi ni mwenzi wa watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.


Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu; Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.


Toka mbele ya uso wa mpumbavu, Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.


Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.


Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;


Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego.


Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.


Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi, Mkaende katika njia ya ufahamu.


Ndipo wale waliomcha BWANA waliposemezana wao kwa wao. Naye BWANA akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha BWANA, na kulitafakari jina lake.


Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.


tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;


Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo