Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 13:19 - Swahili Revised Union Version

19 Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu; Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

19 Inafurahisha upatapo kile unachotaka, kwa hiyo wapumbavu huchukia kuepa uovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

19 Inafurahisha upatapo kile unachotaka, kwa hiyo wapumbavu huchukia kuepa uovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

19 Inafurahisha upatapo kile unachotaka, kwa hiyo wapumbavu huchukia kuepa uovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

19 Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi, bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

19 Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi, bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

19 Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu; Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.

Tazama sura Nakili




Methali 13:19
17 Marejeleo ya Msalaba  

Na tena, mfalme akasema hivi, BWANA, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenipa leo hivi mtu wa kuketi katika kiti changu cha enzi, nayo macho yangu yakiwa yanaona hayo.


Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu.


Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.


Jiepushe na uovu, utende mema, Na kukaa hata milele.


Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.


Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.


Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.


Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu; Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.


Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.


Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.


Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.


Usiwe na hekima machoni pako; Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.


Kitambo kidogo tu nilipoachana nao, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa.


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo