Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 10:21 - Swahili Revised Union Version

21 Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi; Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Maneno ya mwadilifu huwafaa watu wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa akili.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Maneno ya mwadilifu huwafaa watu wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa akili.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Maneno ya mwadilifu huwafaa watu wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa akili.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

21 Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi; Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

Tazama sura Nakili




Methali 10:21
28 Marejeleo ya Msalaba  

Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,


Kinywa chake mwenye haki hunena hekima, Na ulimi wake husema hukumu.


Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha BWANA.


Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.


Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.


Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,


Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.


Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.


Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.


Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?


Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;


Upate kuilinda busara, Na midomo yako iyahifadhi maarifa.


Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.


Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.


Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.


Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.


Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA, Mungu wa majeshi.


nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu.


Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.


Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.


Kila mtu alisikiapo neno la ufalme bila kulielewa, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.


Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.


lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo