Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Samueli 22:29 - Swahili Revised Union Version

29 Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA; Na BWANA ataniangazia giza langu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

29 Ee Mwenyezi-Mungu, wewe u taa yangu, Mungu wangu, unayefukuza giza langu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

29 Ee Mwenyezi-Mungu, wewe u taa yangu, Mungu wangu, unayefukuza giza langu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

29 Ee Mwenyezi-Mungu, wewe u taa yangu, Mungu wangu, unayefukuza giza langu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

29 Wewe ni taa yangu, Ee Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu hulifanya giza langu kuwa mwanga.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

29 Wewe ni taa yangu, Ee bwana. bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

29 Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA; Na BWANA ataniangazia giza langu.

Tazama sura Nakili




2 Samueli 22:29
16 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli.


Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili Daudi, mtumishi wangu, apate kuwa na taa siku zote mbele zangu katika Yerusalemu, mji ule niliouchagua niweke jina langu huko.


Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani, Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;


Nuru huwaangaza wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki.


Kwa kuwa Wewe unaiwasha taa yangu; BWANA Mungu wangu aniangazia giza langu.


BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?


Wengi husema, Nani atakayetuonesha mema? BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Nuru humwangazia mwenye haki, Na furaha ni kwa wanyofu wa moyo.


Ni nani miongoni mwenu amchaye BWANA, aitiiye sauti ya mtumishi wake? Yeye aendaye katika giza, wala hana nuru, naye alitumainia jina la BWANA, na kumtegemea Mungu wake.


Nitaivumilia ghadhabu ya BWANA, kwa kuwa nimemwasi; hata atakaponitetea shutuma yangu, na kunifanyia hukumu; atanileta nje kwenye nuru, nami nitaiona haki yake.


Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawachomozea, likiwa na uwezo wa kuponya katika miale yake; nanyi mtatoka nje, na kuchezacheza kama ndama watokapo mazizini.


Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.


Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.


Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-kondoo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo