Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Samueli 22:22 - Swahili Revised Union Version

22 Maana nimezishika njia za BWANA, Wala sikumwasi Mungu wangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Kwa maana nimezishika njia za Mwenyezi Mungu; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Kwa maana nimezishika njia za bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

22 Maana nimezishika njia za BWANA, Wala sikumwasi Mungu wangu.

Tazama sura Nakili




2 Samueli 22:22
15 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana nimemchagua ili awaamuru wanawe na vizazi vyake baada yake wadumishe njia ya BWANA, kwa kuwa wenye haki na kweli, ili BWANA naye akamtimizie Abrahamu ahadi zake.


na wewe, ukienda mbele zangu kama alivyokwenda Daudi, baba yako, kwa ukamilifu wa moyo, na kwa adili, kufanya hayo yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu,


Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya BWANA.


Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, BWANA atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli.


Heri kila mtu amchaye BWANA, Aendaye katika njia yake.


Wewe, BWANA, nguvu yangu, nakupenda sana;


Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.


Basi, wanangu, nisikilizeni sasa; Maana heri hao wazishikao amri zangu.


na hao waliorudi nyuma, na kuacha kumfuata BWANA; na hao wasiomtafuta BWANA, wala kumwulizia.


Musa akakasirika sana, akamwambia BWANA. Usiikubali sadaka yao; mimi sikutwaa hata punda mmoja kwao, wala sikumwumiza hata mtu mmoja miongoni mwao.


Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.


Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.


Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za BWANA, na mbele ya masihi wake, nilitwaa ng'ombe wa nani? Au nilitwaa punda wa nani? Au ni nani niliyemdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo