Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 81:2 - Swahili Revised Union Version

Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

vumisheni wimbo wa shangwe, pigeni ngoma, chezeni zeze na kinubi cha sauti nzuri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

vumisheni wimbo wa shangwe, pigeni ngoma, chezeni zeze na kinubi cha sauti nzuri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

vumisheni wimbo wa shangwe, pigeni ngoma, chezeni zeze na kinubi cha sauti nzuri.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 81:2
11 Marejeleo ya Msalaba  

hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru BWANA nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu BWANA, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya BWANA,


na Maaseya, na Shemaya, na Eleazari, na Uzi, na Yehohanani, na Malkiya, na Elamu, na Ezeri. Waimbaji wakaimba kwa sauti kuu, akiwa Yezrahia msimamizi wao.


Ee nguvu zangu, nitakuimbia sifa, Maana Ewe Mungu ndiwe ngome yangu, Mungu wa fadhili zangu.


Kwa chombo chenye nyuzi kumi, Na kwa kinanda, Na kwa mlio wa kinubi.


Na Miriamu, nabii mwanamke, dada yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.


Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda katika mlima wa Mizeituni.


mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;


Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.


Kuna mtu miongoni mwenu anayeteseka? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi.