Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yoshua 6:12 - Swahili Revised Union Version

Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, nao makuhani wakalichukua sanduku la BWANA.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Asubuhi yake Yoshua akaamka alfajiri na mapema, na makuhani wakalibeba lile sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Asubuhi yake Yoshua akaamka alfajiri na mapema, na makuhani wakalibeba lile sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Asubuhi yake Yoshua akaamka alfajiri na mapema, na makuhani wakalibeba lile sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yoshua akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, nao makuhani wakalichukua Sanduku la Mwenyezi Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la bwana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, nao makuhani wakalichukua sanduku la BWANA.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yoshua 6:12
11 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.


ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la Agano la BWANA akawaambia,


Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, nao wakatoka Shitimu, wakafika katika mto wa Yordani, yeye na wana wa Israeli wote, wakakaa hapo kabla ya kuvuka.


Basi akalipeleka sanduku la BWANA liuzunguke huo mji, likauzunguka mara moja, kisha wakaenda kambini wakakaa humo kambini.


Na wale makuhani saba wakayachukua mabaragumu saba ya pembe za kondoo dume mbele ya sanduku la BWANA, wakaenda huku wakiyapiga mabaragumu; nao watu wenye silaha wakawatangulia, na hao waliokuwa nyuma wakalifuata sanduku la BWANA; huku makuhani wakiyapiga mabaragumu bila kukoma.


Basi wana wa Israeli waliondoka asubuhi, wakapanga hema zao ili kuvamia Gibea.