Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 14:15 - Swahili Revised Union Version

Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Mkinipenda mtazishika amri zangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Mkinipenda mtazishika amri zangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Mkinipenda mtazishika amri zangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Kama mnanipenda, mtazishika amri zangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Kama mnanipenda, mtazishika amri zangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 14:15
20 Marejeleo ya Msalaba  

Maana alishikamana na BWANA, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake BWANA alizomwamuru Musa.


Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.


Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nilitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma.


Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maranatha.


Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutotahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.


Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usioisha.


Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamumwoni sasa, mnamwamini; na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu,


Na huu ndio upendo: tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende kwayo.