Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Waebrania 12:5 - Swahili Revised Union Version

tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau maonyo ya Bwana, Wala usife moyo ukiadhibiwa naye;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja nyinyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja nyinyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja nyinyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nanyi mmesahau yale maneno ya kuwaonya yanayowataja ninyi kuwa wana, yakisema: “Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala usikate tamaa akikukemea,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nanyi mmesahau yale maneno ya kuwaonya yanayowataja ninyi kuwa wana, yakisema: “Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala usikate tamaa akikukemea,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau maonyo ya Bwana, Wala usife moyo ukiadhibiwa naye;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Waebrania 12:5
33 Marejeleo ya Msalaba  

Kwani kuna mtu aliyemwambia Mungu, Mimi nimevumilia kurudiwa, ingawa sikukosa;


BWANA ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.


Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, Lakini sheria yako sikuisahau.


Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.


Kabla sijateswa mimi nilipotea, Lakini sasa nimelitii neno lako.


Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee BWANA, na kwa uaminifu umenitesa.


Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, Sikuzisahau amri zako.


Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;


Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.


Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.


Hakika nimemsikia Efraimu, akijililia hivi, Umeniadhibu, nami nikaadhibika, kama ndama asiyeizoea nira; unigeuze, nami nitageuka; kwa maana wewe u BWANA, Mungu wangu.


Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?


Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa bado yuko Galilaya,


Wakayakumbuka maneno yake.


Ila tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupasa adhabu pamoja na dunia.


Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.


Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.


Ni kwa ajili ya kuonywa mnastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyeonywa na babaye?


Lakini nawasihi, ndugu, mchukuliane na neno hili lenye maonyo maana nimewaandikia kwa maneno machache.


Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji la uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.


Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.