Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Nahumu 3:9 - Swahili Revised Union Version

Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Puti na Walibya walikuwa wasaidizi wake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kushi ilikuwa nguvu yake; nayo Misri pia, tena bila kikomo; watu wa Puti na Libia waliusaidia!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kushi ilikuwa nguvu yake; nayo Misri pia, tena bila kikomo; watu wa Puti na Libia waliusaidia!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kushi ilikuwa nguvu yake; nayo Misri pia, tena bila kikomo; watu wa Puti na Libia waliusaidia!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kushi na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka; Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kushi na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka; Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Puti na Walibya walikuwa wasaidizi wake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Nahumu 3:9
12 Marejeleo ya Msalaba  

Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.


Wana wa Hamu; Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.


akiwa na magari elfu moja na mia mbili, na wapanda farasi elfu sitini; na watu wasiohesabika, waliotoka Misri pamoja naye; Walubi, na Wasukii, na Wakushi.


Je! Hao Wakushi na Walubi hawakuwa jeshi kubwa mno, wenye magari na wapanda farasi wengi sana? Lakini, kwa kuwa ulimtegemea BWANA, aliwatia mkononi mwako.


Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao.


Haya! Pandeni, enyi farasi; Jihimizeni, enyi magari ya vita; Mashujaa nao na watoke nje Kushi na Puti, watumiao ngao; Nao Waludi, washikao uta na kuupinda.


Watu wa Uajemi na Ludi na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita; walitungika ngao na chapeo ndani yako; wakadhihirisha uzuri wako.


Walipokushika kwa mkono wako, ulivunjika, ukawararua mabega yao yote; nao walipokutegemea, ulivunjika, ukawatetemesha viuno vyao vyote.


Kushi, na Putu, na Ludi, na watu wote waliochanganyika, na Kubu, na wana wa nchi ya agano, wataanguka kwa upanga pamoja nao.


Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri, na jamii ya watu wake, Je! Umefanana na nani katika ukuu wako?


Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo;


Lakini atakuwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibya na Wakushi watafuata nyayo zake.