Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 20:5 - Swahili Revised Union Version

5 Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufadhaika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufadhaika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufadhaika.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao.

Tazama sura Nakili




Isaya 20:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Sasa tazama, unaitumainia fimbo ya mwanzi huu uliopondeka, yaani, Misri, ambayo mtu akiitegemea, humwingia mkononi na kumchoma; ndivyo alivyo Farao, mfalme wa Misri, kwa wote wamtumainio.


Mwacheni mwanadamu ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake; kwa maana wanafaa kitu gani?


Basi, nguvu za Farao zitakuwa aibu yenu, na kutumainia kivuli cha Misri kutakuwa aibu yenu.


Wote watawaonea haya watu wasioweza kuwafaidia, wasio na msaada wala faida, bali ni aibu na sababu ya kushutumiwa.


Kwa maana msaada wa Misri haufai kitu na ni bure; Kwa hiyo nimemwita, “Rahabu aketiye kimya”.


Ole wao wateremkao kwenda Misri wapate msaada, na kutegemea farasi; watumainio magari kwa kuwa ni mengi, na wapanda farasi kwa kuwa ni hodari sana; lakini hawamwangalii Mtakatifu wa Israeli, wala hawamtafuti BWANA!


Tazama, unaitumainia fimbo ya mwanzi huu uliovunjika, yaani, Misri, ambayo, mtu akitegemea juu yake, humwingia mkononi na kumchoma; ndivyo alivyo Farao, mfalme wa Misri, kwa wote wamtumainio.


Wawezaje, basi, kurudisha nyuma uso wa afisa mmoja wa watumishi walio wadogo wa bwana wangu, na kuitumainia Misri upewe magari na farasi?


Naye alisikia habari ya Tirhaka, mfalme wa Kushi, ya kwamba, Ametoka ili kupigana nawe; naye aliposikia hayo, akatuma wajumbe kwa Hezekia, kusema,


BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.


BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitamwadhibu Amoni wa No, na Farao, na Misri, pamoja na miungu yake, na wafalme wake, naam, Farao, na hao wanaomtumainia;


Wala hautakuwa tena tegemeo la nyumba ya Israeli, kufanya maovu yakumbukwe, watakapogeuka kuangalia nyuma yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.


Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Puti na Walibya walikuwa wasaidizi wake.


Na ninyi Wakushi pia, mtauawa kwa upanga wangu.


Basi, mtu yeyote na asijisifie wanadamu. Kwa maana vyote ni vyenu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo