Lutu akatoka na kusema na wachumba wa binti zake, akawaambia, “Ondokeni mahali hapa kwa sababu BWANA atauharibu mji huu”. Lakini akaonekana kama achezaye machoni pa wakwe zake.
Mwanzo 34:9 - Swahili Revised Union Version Mkaoane na sisi, mtupe sisi binti zenu, nanyi mkatwae binti zetu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Acheni tuoane: Nyinyi mtatuoza binti zenu, nasi tutawaoza binti zetu. Biblia Habari Njema - BHND Acheni tuoane: Nyinyi mtatuoza binti zenu, nasi tutawaoza binti zetu. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Acheni tuoane: nyinyi mtatuoza binti zenu, nasi tutawaoza binti zetu. Neno: Bibilia Takatifu Oaneni na sisi; tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu. Neno: Maandiko Matakatifu Oaneni na sisi, tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu. BIBLIA KISWAHILI Mkaoane na sisi, mtupe sisi binti zenu, nanyi mkatwae binti zetu. |
Lutu akatoka na kusema na wachumba wa binti zake, akawaambia, “Ondokeni mahali hapa kwa sababu BWANA atauharibu mji huu”. Lakini akaonekana kama achezaye machoni pa wakwe zake.
nami nitakuapisha kwa BWANA, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao;
Rebeka akamwambia Isaka, Rohoni mwangu sina raha kwa sababu ya hao binti za Hethi. Kama Yakobo akitwaa mke katika binti za Hethi, kama hawa binti za nchi, maisha yangu yatanifaidi nini?
Nanyi mtakaa nasi, na nchi hii itakuwa mbele yenu; kaeni, na kufanya biashara humo, mkapate mali humo.
Hamori akasema nao, akinena, roho ya Shekemu, mwanangu, inamtamani binti yenu, tafadhalini, mpeni amwoe.
wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wowote waliowachagua.
je! Tuzivunje tena amri zako, tukajiunge na watu wanaotenda machukizo hayo, kwa kuoana nao? Je! Usingekasirika nasi hata kutuangamiza kabisa, pasisalie mabaki yoyote, wala mtu wa kuokoka?