Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mika 4:12 - Swahili Revised Union Version

Lakini wao hawayajui mawazo ya BWANA, wala hawafahamu shauri lake; kwamba amewakusanya kama miganda mahali pa kupuria.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini wao hawafahamu mawazo ya Mwenyezi-Mungu wala hawaelewi mpango wake: Kwamba amewakusanya pamoja, kama miganda mahali pa kupuria.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini wao hawafahamu mawazo ya Mwenyezi-Mungu wala hawaelewi mpango wake: Kwamba amewakusanya pamoja, kama miganda mahali pa kupuria.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini wao hawafahamu mawazo ya Mwenyezi-Mungu wala hawaelewi mpango wake: kwamba amewakusanya pamoja, kama miganda mahali pa kupuria.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini hawayajui mawazo ya Mwenyezi Mungu; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini hawayajui mawazo ya bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini wao hawayajui mawazo ya BWANA, wala hawafahamu shauri lake; kwamba amewakusanya kama miganda mahali pa kupuria.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mika 4:12
15 Marejeleo ya Msalaba  

Hulitangaza neno lake kwa Yakobo, Na amri zake na hukumu zake kwa Israeli.


Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo, Wala hukumu zake hawakuzijua. Haleluya.


Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu, na kukatilia mbali mataifa, wala si mataifa machache.


Ewe wangu niliyekufikicha na kukupura; Hayo niliyoyasikia kwa BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, nayatangaza kwenu.


Na wingi wa mataifa wapiganao na Arieli, wote wapiganao naye na ngome yake, na wanaomwudhi, watakuwa kama ndoto, na maono ya usiku.


Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.


Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za baadaye.


Wewe ni rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunjavunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;


Kwa maana BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi; Binti Babeli amekuwa kama sakafu ya kufikichia wakati wa kukanyagwa kwake; bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utafika kwake.


nitakusanya mataifa yote, nami nitawaleta chini katika bonde la Yehoshafati, na huko nitawahukumu kwa ajili ya watu wangu, na kwa ajili ya urithi wangu, Israeli, ambao wamewatawanya kati ya mataifa, na kuigawanya nchi yangu.


ambaye ungo wake uko mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanja wake wa kupuria, na kuikusanya ngano ghalani mwake, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.