Methali 7:12 - Swahili Revised Union Version Mara yuko katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Mara barabarani, mara sokoni, katika kila kona ya njia hakosekani akivizia. Biblia Habari Njema - BHND Mara barabarani, mara sokoni, katika kila kona ya njia hakosekani akivizia. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza mara barabarani, mara sokoni, katika kila kona ya njia hakosekani akivizia. Neno: Bibilia Takatifu mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.) Neno: Maandiko Matakatifu mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.) BIBLIA KISWAHILI Mara yuko katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia. |
Kwa maana tangu zamani wewe umeivunja nira yako, na kuvipasua vifungo vyako; ukasema, Mimi sitatumika; kwa maana juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi, umejiinamisha, ukafanya mambo ya ukahaba.
Jinsi ulivyoitengeneza njia yako ili kutafuta mapenzi! Kwa sababu hiyo hata wanawake wabaya umewafundisha njia zako.
Mbona unatangatanga hivi upate kugeuza mwendo wako? Utaona haya kwa ajili ya Misri pia, kama ulivyoona haya kwa ajili ya Ashuru.
Inua macho yako, ukavitazame vilele vya milima, ukaone; pako wapi mahali ambapo hawakulala nawe? Kando ya njia umeketi ili kuwangojea, kama vile Mwarabu jangwani; nawe umeitia nchi unajisi kwa ukahaba wako na uovu wako.
apendaye kutawala watu; kwa kuwa wajijengea mahali pako pakuu penye kichwa cha kila njia, na kufanya mahali pako palipoinuka katika kila njia kuu; lakini hukuwa kama kahaba, kwa maana ulidharau kupokea ujira.
wala nuru ya taa haitamulika ndani yako tena kabisa; wala sauti ya bwana arusi na bibi arusi haitasikika ndani yako tena kabisa; maana hao wafanya biashara wako walikuwa wakuu wa nchi, kwa kuwa mataifa yote walidanganywa kwa uchawi wako.
kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.