Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:16 - Swahili Revised Union Version

Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waovu wakitawala maovu huongezeka, lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waovu wakitawala maovu huongezeka, lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waovu wakitawala maovu huongezeka, lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Waovu wanapostawi, dhambi huongezeka pia; lakini wenye haki wataliona anguko lao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:16
11 Marejeleo ya Msalaba  

Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa.


Wewe umngoje BWANA, Uishike njia yake, Naye atakutukuza uirithi nchi, Utawaona Wasio haki wakiangamizwa.


Nikapita na kumbe! Hayuko, Nikamtafuta wala hakuonekana.


Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.


Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.


Na jicho langu limeona kuanguka kwa adui zangu, Sikio langu limesikia maangamizi ya waovu walionishambulia.


Maana hao adui zako, Ee BWANA, Hao adui zako watapotea, Na watendao maovu watatawanyika wote pia.


Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya; Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.


Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.


Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.


Furahini juu yake, enyi mbingu, na enyi watakatifu, mitume na manabii; kwa maana Mungu ametoa hukumu kwa ajili yenu juu yake.