Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 24:21 - Swahili Revised Union Version

Mwanangu, mche BWANA, na mfalme; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme, wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme, wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme, wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwanangu, mche Mwenyezi Mungu na mfalme, wala usijiunge na waasi,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwanangu, mche bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwanangu, mche BWANA, na mfalme; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 24:21
16 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga.


Ndipo wageni wote waliokuwa pamoja na Adonia wakaogopa, wakaondoka, wakaenda zao kila mtu njia yake.


Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli wakaenda zao hemani kwao.


Israeli akaiona ile kazi kubwa aliyoifanya BWANA juu ya Wamisri, ndipo hao watu wakamcha BWANA, wakamwamini BWANA, na Musa mtumishi wake.


Mtu mwovu hataki neno ila kuasi tu; Kwa hiyo mjumbe mkali atatumwa kwake.


Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi; Bali mche BWANA mchana kutwa;


Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.


Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa watawala na wenye mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema;


Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa BWANA.