Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 23:30 - Swahili Revised Union Version

Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ni wale ambao hawabanduki penye divai, wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ni wale ambao hawabanduki penye divai, wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ni wale ambao hawabanduki penye divai, wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ni hao wanaokaa sana kwenye mvinyo, hao wanaoenda kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 23:30
10 Marejeleo ya Msalaba  

akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.


Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.


Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.


Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.


Amechinja nyama zake, amechanganya divai yake, Ameiandalia meza yake pia.


Lakini hawa nao wamekosa kwa divai, wamepotea kwa kileo; kuhani na nabii wamekosa kwa kileo, wamemezwa kwa divai, wamepotea kwa kileo; hukosa katika maono, hujikwaa katika hukumu.


Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hadi usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao!


ninyi mnaokunywa divai katika mabakuli, na kujipaka marhamu iliyo nzuri; lakini hawahuzuniki kwa sababu ya mateso ya Yusufu.


Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;


Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hadi kulipopambazuka.