Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 4:19 - Swahili Revised Union Version

Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya nyinyi wavuvi wa watu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya nyinyi wavuvi wa watu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya nyinyi wavuvi wa watu.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 4:19
17 Marejeleo ya Msalaba  

Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.


Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, nenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.


Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.


Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.


Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.


Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata.


Na alipokuwa akipita, akamwona Lawi wa Alfayo, ameketi forodhani, akamwambia, Nifuate. Akaondoka akamfuata.


Baada ya hayo akatoka, akaona mtoza ushuru, jina lake Lawi, ameketi forodhani, akamwambia, Nifuate.


Akamwambia mwingine, Nifuate. Akasema, Bwana, nipe ruhusa kwanza niende nikamzike baba yangu.


Kesho yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.


Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.


Yesu akamwambia, Ikiwa nataka huyu akae hata nitakapokuja, imekuhusuje wewe? Wewe unifuate mimi.


Lakini na iwe hivyo, mimi sikuwalemea; bali kwa kuwa mwerevu niliwapata kwa hila.