Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 27:52 - Swahili Revised Union Version

makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 27:52
13 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu.


Amemeza mauti hata milele; na Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote; na aibu ya watu wake ataiondoa katika ulimwengu wote; maana BWANA amenena hayo.


Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana umande wako ni kama umande wa mimea, nayo ardhi itawatoa waliokufa.


Tena, wengi wa hao wanaolala katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.


Nitawakomboa kwa nguvu za kaburi; nitawaokoa kutoka kwa mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Huruma itafichika machoni mwangu.


Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.


Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona kitendo cha kuuawa kwake kuwa sawa.


Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio wagonjwa na dhaifu, na watu kadhaa wamelala.


Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.


Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,


Maana, ikiwa tunaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.


ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tunakesha au tunalala.