Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 27:50 - Swahili Revised Union Version

Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 27:50
14 Marejeleo ya Msalaba  

Na baada ya yale majuma sitini na mawili, masihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa.


kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.


Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.


Naye Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.


Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.


Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.


kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.


Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani.


Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.


Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,


Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;


basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na dosari, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?