Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 26:70 - Swahili Revised Union Version

Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 26:70
17 Marejeleo ya Msalaba  

Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.


Tena ni nani uliyemwogopa na kumhofu, hata ukasema uongo, wala hukunikumbuka mimi, wala kuweka hayo moyoni? Je! Mimi sikunyamaza tangu zamani, hata huniogopi?


Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?


Na tazama, mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.


Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.


Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho.


Na Petro alikuwa ameketi nje uani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya.


Naye alipotoka nje hadi ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti.


Akakana, akisema, Ee mwanamke, simjui.


Vema. Yalikatwa kwa kutoamini kwao, na wewe wasimama kwa imani yako. Usijivune, bali uogope.


Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.


Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.