Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Marko 2:25 - Swahili Revised Union Version

Akawaambia, Hamkusoma popote alivyofanya Daudi, alipokuwa akiona njaa na kuhitaji chakula, yeye na wenziwe?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi yeye na wenzake walipokuwa na njaa, wakahitaji chakula?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akawaambia, Hamkusoma popote alivyofanya Daudi, alipokuwa akiona njaa na kuhitaji chakula, yeye na wenziwe?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Marko 2:25
11 Marejeleo ya Msalaba  

Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mwanamume na mwanamke,


wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umejiandalia sifa?


Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni la ajabu machoni petu?


Tena kuhusu kiyama ya wafu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema,


Akafunga siku arubaini mchana na usiku, mwishowe akaona njaa.


Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzawa.


Na kuhusu wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Kuhusu kile kichaka jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Abrahamu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?


Mafarisayo wakamwambia, Tazama, mbona wanafanya lisilokuwa halali siku ya sabato?


Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu, akaila mikate ile ya wonyesho, ambayo si halali kuliwa ila na makuhani, akawapa na wenziwe?


Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?