Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Marko 13:23 - Swahili Revised Union Version

Bali ninyi jihadharini; nimekwisha kuwaonya yote mbele.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini nyinyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini nyinyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini nyinyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Bali ninyi jihadharini; nimekwisha kuwaonya yote mbele.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Marko 13:23
13 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.


Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali.


kwa maana watajitokeza Makristo wa uongo, na manabii wa uongo, watatoa ishara na maajabu, wapate kuwadanganya, ikiwezekana, hata hao wateule.


Lakini siku zile, baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hatautoa mwanga wake.


Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.


Yesu akaanza kuwaambia, Jihadharini, mtu asiwadanganye.


Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.


Basi, jihadharini, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafla, kama mtego unasavyo;


Akasema, Angalieni, msije mkadanganyika, kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ndiye; tena, Majira yamekaribia. Basi msiwafuate hao.


Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, ili litakapotokea mpate kuamini.


Basi, wapenzi kwa kuwa mmejua hayo, jihadharini msije mkapotoshwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthabiti wenu.