Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:42 - Swahili Revised Union Version

Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Sisi tulikukosea na kukuasi nawe bado hujatusamehe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Sisi tulikukosea na kukuasi nawe bado hujatusamehe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Sisi tulikukosea na kukuasi nawe bado hujatusamehe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:42
16 Marejeleo ya Msalaba  

tena kwa ajili ya damu zisizo na hatia alizozimwaga; kwani aliujaza Yerusalemu damu zisizo na hatia; wala BWANA hakukubali kusamehe.


nikasema, Ee Mungu wangu, nimetahayari, naona haya kuinua uso wangu mbele zako, Mungu wangu; kwa maana maovu yetu ni mengi, hata yamefika juu ya vichwa vyetu, na hatia yetu imeongezeka na kufika mbinguni.


Walakini hawakukutii, wakakuasi, wakaitupa sheria yako nyuma yao, wakawaua manabii wako waliowaonya ili wapate kukurudia wewe; wakakufuru sana.


Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye Juu.


Ee BWANA, tunakiri uovu wetu, na ubaya wa baba zetu; maana tumekutenda dhambi.


Ungama uovu wako tu; ya kwamba umemwasi BWANA, Mungu wako, na njia zako zimekuwa nyingi kuwaendea wageni chini ya kila mti wenye majani mabichi, wala hamkuitii sauti yangu, asema BWANA.


BWANA ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.


Taji ya kichwa chetu imeanguka; Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.


Katika uchafu wako mna uasherati, kwa maana nimekusafisha, ila wewe hukusafika; hutasafishwa tena uchafu wako ukutoke, hadi nitakapokuwa nimeituliza hasira yangu kwako.


Na sasa, Ee Bwana Mungu wetu, uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama ilivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu.


Je, Baba zenu wako wapi? Je, manabii nao wanaishi milele?


Lakini maneno yangu, na amri zangu nilizowaagiza hao manabii, watumishi wangu, je, Hazikuwapata baba zenu? Nao wakatubu na kusema, BWANA wa majeshi ametutenda kulingana na njia zetu, na matendo yetu, kama alivyokusudia kutenda.