Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 24:6 - Swahili Revised Union Version

Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa bado yuko Galilaya,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa bado yuko Galilaya,

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 24:6
19 Marejeleo ya Msalaba  

Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.


Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.


wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa angali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.


Hayupo hapa; maana amefufuka kama alivyosema. Njooni, mpatazame mahali alipolazwa.


Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka.


Akaanza kuwafundisha kwamba imempasa Mwana wa Adamu kupatikana na mateso mengi, na kukataliwa na wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na baada ya siku tatu kufufuka.


wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.


nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hadi nchini, hao waliwaambia, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?


akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa na siku ya tatu kufufuka.


Yashikeni maneno haya masikioni mwenu, kwa kuwa Mwana wa Adamu anakwenda kutiwa katika mikono ya watu.


ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.


Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi niliwaambia hayo?