Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 24:11 - Swahili Revised Union Version

hao waliwaambia mitume habari ya mambo hayo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

hao waliwaambia mitume habari ya mambo hayo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 24:11
10 Marejeleo ya Msalaba  

Lutu akatoka na kusema na wachumba wa binti zake, akawaambia, “Ondokeni mahali hapa kwa sababu BWANA atauharibu mji huu”. Lakini akaonekana kama achezaye machoni pa wakwe zake.


Basi yule afisa, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama BWANA angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.


Kama ningemwita, naye akaniitikia; Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.


BWANA alipowarejesha mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto.


Lakini hao waliposikia kwamba yu hai, naye amemwona, hawakuamini.


Na hao wakaenda zao wakawapa habari wale wengine; wala hao hawakuwaamini.


Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutoamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu.


Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!


Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula chochote hapa?


Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.