Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 17:3 - Swahili Revised Union Version

Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa hiyo, jilindeni. “Ndugu yako akikukosea, mwonye; naye akitubu, msamehe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 17:3
18 Marejeleo ya Msalaba  

Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.


Ujihadhari nafsi yako, usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi ile unayoiendea, lisiwe mtego katikati yako.


Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu, Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.


Lawama ya wazi ni heri, Kuliko upendo uliositirika.


Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.


Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, au ulipizwe uovu kwa ajili yake


Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?


Basi, jihadharini, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafla, kama mtego unasavyo;


Basi angalieni sana jinsi mnavyoenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;


Jihadharini nafsi zenu basi; maana hamkuona umbo la namna yoyote siku ile BWANA aliyosema nanyi kutoka kati ya moto;


Jihadharini nafsi zenu, msije mkalisahau agano la BWANA, Mungu wenu, alilolifanya nanyi, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu chochote ulichokatazwa na BWANA, Mungu wenu,


Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako;


mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.


Ndugu zangu, mtu yeyote miongoni mwenu akipotoka mbali na kweli, na kurejeshwa na mtu mwingine;


Jiangalieni nafsi zenu msiyapoteze mliyoyatenda, bali mpokee thawabu timilifu.