Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hosea 8:12 - Swahili Revised Union Version

Nijapomwandikia sheria yangu katika amri makumi elfu, zimehesabiwa kuwa ni kitu kigeni.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi, wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi, wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi, wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Niliwaandikia mambo mengi yaliyohusu sheria yangu, lakini waliziangalia kama kitu kigeni.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi kuhusu sheria yangu, lakini wameziangalia kama kitu cha kigeni.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nijapomwandikia sheria yangu katika amri makumi elfu, zimehesabiwa kuwa ni kitu kigeni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hosea 8:12
14 Marejeleo ya Msalaba  

Walakini hawakukutii, wakakuasi, wakaitupa sheria yako nyuma yao, wakawaua manabii wako waliowaonya ili wapate kukurudia wewe; wakakufuru sana.


Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako.


Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.


Je! Sikukuandikia mambo makuu juu ya mashauri na juu ya maarifa;


Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya BWANA;


Nikawapa amri zangu, na kuwaonesha hukumu zangu, ambazo mwanadamu ataishi kwazo, kama akizitenda.


Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.


Basi Myahudi ana nini zaidi? Na kutahiriwa kwafaa nini?


Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.