Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 5:22 - Swahili Revised Union Version

Na wewe, mwanawe, Ee Belshaza, hukujinyenyekeza moyo wako, ijapokuwa ulijua hayo yote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini wewe Belshaza, mwanawe, ingawa unayajua haya yote, hukujinyenyekeza!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini wewe Belshaza, mwanawe, ingawa unayajua haya yote, hukujinyenyekeza!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini wewe Belshaza, mwanawe, ingawa unayajua haya yote, hukujinyenyekeza!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Nawe Belsasari u mwanawe, lakini hukuunyenyekeza moyo wako, ingawa uliyajua hayo yote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 5:22
17 Marejeleo ya Msalaba  

Wala hakujinyenyekeza mbele za BWANA, kama Manase babaye alivyojinyenyekeza; lakini huyo Amoni akaongeza makosa juu ya makosa.


akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA, Mungu wake; wala hakujinyenyekeza mbele ya Yeremia nabii aliponena kwa kinywa cha BWANA.


Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.


Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie.


Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayashusha chini majivuno yao walio wakali;


Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.


Mtu mbaya ajapofadhiliwa, Hata hivyo hatajifunza haki; Katika nchi ya unyofu atatenda udhalimu, Wala hatauona utukufu wa BWANA.


Kwa habari zako, Ee mfalme, Mungu Aliye Juu alimpa Nebukadneza, baba yako, ufalme, na ukuu, na fahari, na utukufu;


Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.


Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.


Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.


Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.


Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.