Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Samueli 8:15 - Swahili Revised Union Version

Daudi akatawala juu ya Israeli wote; naye Daudi akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hivyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, akahakikisha watu wake wote wanatendewa haki ipasavyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hivyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, akahakikisha watu wake wote wanatendewa haki ipasavyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hivyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, akahakikisha watu wake wote wanatendewa haki ipasavyo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Daudi akatawala juu ya Israeli yote; naye akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Samueli 8:15
24 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza.


Basi Yoabu alikuwa akiongoza jeshi lote la Israeli; na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa akiwaongoza Wakerethi, na Wapelethi;


Basi Abneri akatuma wajumbe kwa Daudi mahali alipokuwapo, akisema, Nchi hii ni ya nani? Fanya agano nami, na tazama, mkono wangu utakuwa pamoja nawe, ili kuwaleta Israeli wote kwako.


Huko Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita; na katika Yerusalemu alitawala miaka thelathini na tatu juu ya Israeli wote na Yuda.


Akaweka askari wenye kulinda ngome katika Edomu; katikati ya Edomu yote akaweka ngome, na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye BWANA akampa Daudi ushindi kila kokote alikokwenda.


Huyo Yoabu, mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa majeshi; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, mwekaji kumbukumbu;


Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti cha enzi cha Israeli; kwa kuwa BWANA amewapenda Israeli milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme, ufanye hukumu na haki.


Basi mfalme Sulemani akawa mfalme juu ya Israeli wote.


Basi Daudi akawatawala Waisraeli wote; akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.


Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.


Atawaamua watu wako kwa haki, Na watu wako walioonewa kwa hukumu.


Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.


Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zimo mbele za uso wako.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba BWANA, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.


Lakini hukumu na iteremke kama maji, na haki kama maji makuu.


ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,


Basi Sauli alipokwisha kuutwaa ufalme juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote pande zote, juu ya Moabu, na juu ya wana wa Amoni, na juu ya Edomu, na juu ya wafalme wa Soba, na juu ya Wafilisti; na popote alipogeukia, akawashinda.