Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Samueli 2:7 - Swahili Revised Union Version

BWANA hufukarisha mtu, na hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu huwafanya baadhi wawe maskini, na baadhi wawe matajiri. Wengine huwashusha, na wengine huwakweza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu huwafanya baadhi wawe maskini, na baadhi wawe matajiri. Wengine huwashusha, na wengine huwakweza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu huwafanya baadhi wawe maskini, na baadhi wawe matajiri. Wengine huwashusha, na wengine huwakweza.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenyezi Mungu humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA hufukarisha mtu, na hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Samueli 2:7
17 Marejeleo ya Msalaba  

Akainuka akaingia nyumbani; naye akayamimina yale mafuta kichwani mwake, akamwambia, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa BWANA, yaani, juu ya Israeli.


Utajiri na heshima hutoka kwako wewe, nawe watawala juu ya vyote; na mkononi mwako mna uweza na nguvu; tena mkononi mwako mna kuwatukuza na kuwawezesha wote.


Naye Hezekia akawa na mali nyingi mno na heshima; akajitengenezea hazina za fedha, za dhahabu, za vito, za manukato, za ngao, na za namna zote za vyombo vya thamani;


Tena akajitengenezea miji, na mali za kondoo na ng'ombe kwa wingi; maana Mungu alimtajirisha sana sana.


akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nikiwa uchi, nami nitarudi tena huko uchi vile vile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.


Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo.


Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.


Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; Maana umeniinua na kunitupilia mbali.


Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu.


Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.


Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.


Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.


Maana nimekufanya mdogo kati ya mataifa, Na kudharauliwa katika watu.


Na miti yote ya mashamba itajua ya kuwa mimi, BWANA, nimeushusha chini mti mrefu, na kuuinua mti mfupi, na kuukausha mti mbichi, na kuusitawisha mti mkavu; mimi, BWANA, nimenena, nami nimelitenda jambo hili.


Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.