Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zekaria 5:9 - Swahili Revised Union Version

9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Nilipotazama juu, niliona wanawake wawili wanatokea kunijia; walikuwa wakirushwa na upepo, nao walikuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. Wanawake hao wakakiinua kile kikapu angani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Nilipotazama juu, niliona wanawake wawili wanatokea kunijia; walikuwa wakirushwa na upepo, nao walikuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. Wanawake hao wakakiinua kile kikapu angani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Nilipotazama juu, niliona wanawake wawili wanatokea kunijia; walikuwa wakirushwa na upepo, nao walikuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. Wanawake hao wakakiinua kile kikapu angani.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, palikuwa na wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, walikuwepo wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.

Tazama sura Nakili




Zekaria 5:9
9 Marejeleo ya Msalaba  

Humo ndege hujenga viota vyao, Korongo, anayo makao katika misonobari.


Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za BWANA.


Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya BWANA; kwa sababu wamelivunja agano langu, wameiasi sheria yangu.


Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;


na korongo, na koikoi kwa aina zake, na hudihudi, na popo.


Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii?


Kwa kuwa popote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.


BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo