Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 10:11 - Swahili Revised Union Version

11 Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, Auficha uso wake, haoni kamwe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Mwovu huwaza moyoni mwake: “Mungu amesahau; ameficha uso wake, haoni kitu!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Mwovu huwaza moyoni mwake: “Mungu amesahau; ameficha uso wake, haoni kitu!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Mwovu huwaza moyoni mwake: “Mungu amesahau; ameficha uso wake, haoni kitu!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau, huficha uso wake na haoni kabisa.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau, huficha uso wake na haoni kabisa.”

Tazama sura Nakili




Zaburi 10:11
13 Marejeleo ya Msalaba  

Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.


Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote.


Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Wakisema, Ni nani atakayeiona?


Ni nani atambuaye maovu yetu? Tumepanga njama kwa werevu mwingi, Maana katika moyo wa mtu na fikira mengi yamefichika.


Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?


Nao husema, BWANA haoni; Mungu wa Yakobo hatambui.


Kwa sababu hukumu juu ya tendo baya haitekelezwi upesi, mioyo ya wanadamu huthibitishwa ndani yao ili kutenda mabaya.


Kisha akaniambia, Mwanadamu, umeyaona wanayotenda wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mtu ndani ya vyumba vyake vya sanamu? Maana husema, BWANA hatuoni; BWANA ameiacha nchi hii.


Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, BWANA ameiacha nchi hii, naye BWANA haoni.


Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu.


Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,


Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo